Thursday, March 31, 2016

SHEIKH ALHAJI RASHID TATASHAJARA ABUBAKAR WA MSIKITI WA MTAA WA MWANZA ILALA DAR ES SALAAM AOKOKA






1. AKIRI KULA NYAMA ZA WATU
2. AKIRI KUNYWA DAMU ZA WATU
3. AKIRI KUMEZA MAJINI 360
4. ASEMA UISLAM NI DINI YA WACHAWI
Ndugu msomaji,
Soma huu ushuhuda wa kusisimua kutoka kwa Sheikh Alhaji Rashid Tatashajara Abubakar aliye kunywa damu za watu, kuhamisha nyota za watu, na kumeza majini 360.
Mwenyekiti wa waislamu waliookoka, Afrika Mashariki na Kati!
Alitokea kwenye familia ya kichawi, mama yake alijiita ni Mungu na kufanya miujiza mbalimbali ikiwemo ya kunyesha mvua. Sheikh Alhaji Rashid Tatashajara Abubakar, aliwahi kufanya shughuli za kisheikh katika msikiti wa Ilala mtaa wa Mwanza ambapo pia alikua mwanafunzi wa sheikh Yahaya Hussein ambaye ni marehemu kwa sasa.
Alianza kujifunza madrasa, akapanda vyeo na kusomea vyuo vya kichawi baada ya kuhitimu majaribio mbalimbali ikiwemo kufukua makaburi, kunywa damu za watu, kuhamisha nyota za watu, na kumeza majini 360 na kufanikiwa kuchaguliwa kuwa mwenyekiti mkuu wa wachawi Afrika mashariki na kati!
Anasema katika mambo hayo yote, alikua akitumwa kushambulia watumishi wa Mungu mbalimbali, aliwahi kujaribu kwa Moses Kulola, Emmanuel Lazaro na Askofu Mwanisongole. Lakini alishindwa na kupata mieleka iliyompelekea kuumwa sana.
Akielezea ushuhuda wake kwa ufupi, Jinsi alivyompokea Bwana Yesu, ilikuwa sababu ya mke wake wa pili kupita kwenye mkutano wa Injili na kuponywa tumbo lililomsumbua kwa muda mrefu bila mafanikio ya kupona “mke wangu alikuwa akirudi nyumbani na kuimba nyimbo za makafiri, baadaye anaenda kanisani, sasa adhabu ya mtu anayekiuka sheria ni viboko 40, nilipotaka kumchapa mkono ukaganda, ndio mke wangu akasema piga magoti chini, akaniombea na mkono ukarudi mahala pake, baada ya hapo mengi yalitokea kukatisha story Mungu alianza kunifundisha na kunitumia”
“Siku Moja mtaa wa Salender Bridge kama mliwahi kusikia kisa cha dada aliyeota manyoya, alifikishwa kwangu nikamuombea kwa Jina la Yesu naye akapokea uponyaji. Kwa sasa yuko Marekani! nimemuona Mungu kwa jinsi ya tofauti kule nilikotoka nilikua namtumikia shetani, kwa sasa namtumikia Bwana Yesu, na kila ulimi utakiri kwamba Yesu ndiye Mungu”
Alhaji Rashid Abubakary kwa sasa ni mwenyekiti wa waislamu waliookoka Afrika mashariki na kati. Mungu amekua akimtumia kwa jinsi ya tofauti na amealikwa makanisa mbalimbali na kueleza shuhuda nyingi ambazo Bwana Yesu amefanya na kufanya kwenye maisha ya watu wengine. Ameonekana kwenye Televisheni ya kikristo ATN, ushuhuda huu kwa ufupi ameutoa tarehe 26 Agosti 2011, Kanisa la City Christian Centre.
By permission
Max Shimba Ministries Org

ABUU MTOTO WA SHEKHE "MUARABU" AKATA SHAURI NA KUMPOKEA YESU

Abuu kwenye ubatizo wa maji mengi chini ya kanisa la EAGT Mito ya Baraka, Dar es Salaam



























1. ABATIZWA NA SASA ANAITWA BOAZ
2. BABA YAKE ANAYEISHI OMAN AKIRI KUWA MUNGU WA "ABUU" HAKIKA NDIE MUNGU MKUU
3. ABUU SASA ANAMTUMIKIA YESU
Ndugu msomaji,
Bwana Yesu apewe sifa,
Haya msomaji wetu karibu katika kipengele chetu maalumu ''USHUHUDA'' ambacho kinakujia kila siku kikiwa na lengo la kukupatia habari ambayo iliwahi kutokea lakini yawezekana hauijui pia yawezekana ilitokea ukawa unaijua lakini labda umesaihau.
Abuu Levy au waweza kumuita kwa jina la Boaz kama wengi walivyomzoea, ni jina ambalo amelipata baada ya ubatizo. Historia yake inarejea kwenye Uislamu, ambako ndipo alilpotokea, asili yake akiwa Muarabu. Baba yake mzazi anaishi Oman hadi hivi sasa.
Kwa taarifa yako, licha ya kukulia kwenye famlia ya usilamu, lakini hakuwai si tu kwenda msikitini, bali pia hata mazingira ya ndani ya msikiti anayafahamu yalivyo. Neema imetokana pale alipolelewa na mama yake mkubwa ambaye ni "mlokole".
Alipotimiza umri wa miaka kumi, Abuu alikata shauri na kuokoka. Lakini pamoja na baba yake mzazi kuwa Shekhe wa imani kali ya Kiislam, hakuleta kipingamizi chochote zaidi ya kumsihi tu kuwa asimuache Mungu, yaani Yesu Kristo. Hii ni tofauti na wazazi wengine wa Kiislam ambapo huleta vita kwa mwanao na hata kutishia kifo.
Pamoja na kupewa baraka na baba yake mzazi ambaye ni Muislam mwenye siasa kali, bado hali haikuwa nyepesi kwa baadhi ya ndugu zake, kwani Abuu amepitia magumu mengi, kuotka ndugu zake ambao takribani wote ni Waislam kwa kumtishia maisha yake na kusema maneno makali yenye laana kwasabu ya kubadili dini na kuwa Mkristo. Hata hivyo Abuu alisimama ndani ya Yesu na hakukuwa na kurudi nyuma. Abuu sasa anamtumikia Yesu kwa kuimba Nyimbo za Injili. Tumeweka linkhttps://www.youtube.com/watch?v=sFu6socEVMQ ya nyimbo zake. Tafadhali nunua CD'S/DVDS zake ili kuendelea kuimarisha kazi yake kwa Bwana wetu Yesu Kristo.
Abuu, mwenye umri wa miaka 24 kwa sasa ni mwimbaji wa nyimbo za injili kwa muda wa miaka nane huku akiwa na album tatu hadi sasa, kati yake mbili zikiwa madukani tayari.
Mungu huandaa na kubadilisha watu wake kwa njia mbalimbali, maana ametujua tangia hatujazaliwa. Naye Abuu yuko kwenye kazi/huduma ya Mungu. Yuko katika utumishi wa Yehova.
Mungu akubariki sana msomaji wetu, tuendelee kuitangaza Injili ya Yesu Kristo kwa Mataifa Yote.
Mungu anawapenda wote na tusikate tamaa hata tunapo kuwa katika magumu, mateso, Yesu bado anatupenda na yupo pamoja nasi kila siku.
Mungu awabariki sana.
By permission
Ni mimi Max Shimba, mtumwa wa Yesu Kristo,
For Max Shimba Ministries Org,
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2016. ALL RIGHTS RESERVED
Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.
April 1, 2016








Monday, March 28, 2016

Nini kitaingia PEPONI: Roho/Nafsi au Mwili au zote mbili?

UTATA MKUMBWA NDANI YA KORAN
Nini kitaingia PEPONI: Roho/Nafsi au Mwili au zote mbili?
Somo letu la leo ni la swali kwa Allah ambaye ameshindwa kujieleza, kuwa ni kipi kinaingia Peponi kati ya Roho/Nafsi au Mwili?
Koran inadai kuwa, baada ya ufufuo, ni mwili (baada ya kuungana na roho?) Ambayo inaingia peponi. Haya madai yamewekewa mkazo katika Koran. Angalia mistari ifuatayo 13:05, 17:98-99, 20:55, 34:7, 75:3-4.
Hata hivyo mistari ya 27-30 kwenye Sura 89 inapinga aya zilizo pita kwa kusema kuwa ni nafsi (Nafs) tu ambayo inaingia Peponi!
Quran 17:99. Kwani hawakuona ya kwamba Mwenyezi Mungu aliye umba mbingu na ardhi ni Mwenye kuweza kuumba mfano wao? Na Yeye amewawekea muda usio na shaka yoyote. Lakini madhaalimu hawataki ila ukafiri.
Quran 75:3. Anadhani mtu kuwa Sisi hatutaikusanya mifupa yake? 4. Kwani! Sisi tunaweza hata kuziweka sawa sawa ncha za vidole vyake!
Aya hizo hapo juu, zinadai kuwa Nafsi na Mwili vitaungana na kuingia Peponi, hayo ni maneno ya Allah kama alivyo yashusha kupitia Quran yake. Lakini Allah huyohuyo anabadilika na kusema kuwa Nafsi ndio itaingia Peponi. Hebu soma aya zifuatazo.
Quran 89 27. Ewe nafsi iliyo tua! 28. Rejea kwa Mola wako Mlezi umeridhika, na umemridhisha.
Katika aya hapo juu, Allah anaiamuru Nafsi irejee kwake. Sasa ni ipi kati ya Nafsi na Mwili vitaingia Peponi? Utata huu ni Msiba Mkubwa kwa Allah ambaye hafahamu nini kati ya Nafsi na Mwili vitaingia Peponi.

UTATA NDANI YA QURAN. "AYA ZA QURAN ZAPINGANA"



Ndugu msomaji,
Leo tutaangali utata mkubwa uliopo kwenye Quran kama ifuatavyo:
Sura Al-Baqara 2:109
109. Wengi miongoni mwa watu wa Kitabu wanatamani lau wange kurudisheni nyinyi muwe makafiri baada ya kuamini kwenu, kwa ajili ya uhasidi uliomo ndani ya nafsi zao, baada ya kwisha wapambanukia Haki. Basi sameheni na wachilieni mbali mpaka Mwenyezi Mungu atapo leta amri yake. Hakika Mwenyezi Mungu ni Muweza wa kila kitu.
Hapa quran inaongelea watu wa kitabu (yaani Wakristo), na kusema:
Wengi wa watu wa kitabu, kutokana na wivu wao, wanatamani kuwarudisheni kwenye kutoamini baada ya kuwa mmeamini, pamoja na kwamba ukweli umeshadhihirishwa wazi mbele yao. Kwa hiyo wasameheni na kuwavumilia hadi Allah atakapowafunulia mapenzi yake. Yeye ana nguvu juu ya kila kitu.
Quran pia inawaagiza Waislamu katika sura Al Imran 3:20 kwamba:
Na pindi wakikuhoji, basi sema: Mimi nimeusalimisha uso wangu kumwelekea Mwenyezi Mungu, na kadhaalika walio nifuata. Na waambie walio pewa Kitabu na wasio na kisomo: Je! Mmesilimu? Wakisilimu basi wameongoka. Na wakikengeuka basi juu yako ni kufikisha ujumbe tu. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kuwaona waja wake.
Yaani:
... kama wasipowasikiliza, basi ninyi kazi yenu pekee ni kuwaonya tu.
Kwa hiyo, kutokana na aya hizi mbili, yaani Al-Baqara 2:109 na Al Imran 3:20, tunaona mambo yafuatayo:

KWANINI ALLAH NA MUHAMMAD (S.A.W) WALIRUHUSU KUUWAWA KWA WAKONGWE NA AJUZA?


Ndugu msomaji,
Leo tutaangalia tabia mbaya ya Allah na Mtume wake Muhammad. Hivi kwanini Allah aliruhusu kuuwawa kwa Vikongwe? Hivi kwanini Muhammad alifanya hiyo kazi ya Allah na kuwauwa Vikongwe na ajuza?
Mohammad na kikosi chake kiliuwa wazee wa makamo; Umm Qirfa Fatima, Abu Afak na mzee aliyekataa kusujudia Al-Kaaba.
Baada ya kuuteka mji wa Kaaba Mohammad alimtuma mfuasi wake, Zayd Ibn Haritha kuenda kuuteka kabila ambalo liliukana Uislamu. Zayd bin Haritha alifanikiwa kuuteka huo mji pamoja na kuuwa wazee wakongwe na kuwateka wanawake na watoto walitojaribu kutoroka.
“…na tuliwashambulia kutoka pande zote hadi tukafika karibu na visima vyao ambapo tulipigana vita vikali. Tuliwauwa Aadui zetu wengine huku wengine wakichukuliwa kama mateka wa vita. Niliona kwa mbali kundi la watu lililojumuisha wanawake na watoto wakitoroka. Niliogopa, wasije wakafike mlimani kabla yangu, hivyo nikalenga mshale kati yao na ukaangukia kwa mbele kati yao na mlima. Nikawarudisha nikiwakimbiza kama mifugo walikotoka. (Sahin Muslim 4345)
Umm Qirfa ni miongoni mwa wanawake walitekwa vitani
Alikuwa ajuza (bi kizee), mke wa Malik. Binti yake (na wenzake) walitekwa pia. Zayd Ibn Haritha akaamuru Qays kuuwa Umm Qirfa na akamuuwa kinyama kwa kumfunga kwa kamba kila mguu kwa ngamia mbili na kuwaamuru hao ngamia kuenda pande tofauti. Umm Qirfa alichanika katikati, akatokwa na damu akapasuka mishipa, mifupa na kufa ghafla! (Ibn Ishaq/Hisham 980)
Binti yake ajuza, Umm Qirfa Fatima, aliletwa Makka pamoja na mateka wengine ambapo alipewa kama jizya (zawadi). (Hii ilikuwa kabla ya Mohammad kumtambua)
Niliwatembeza hadi nikawaleta kwa Abu Bakr ambaye alinitunukiza huyu binti kama zawadi. Hivyo tukafika Medina. Sikuwa nimemvua buibui wakati mtume wa Allah (s.a.w) alipokutana nami njiani na kusema; “nipe huyu binti awe mke wangu.” (Sahih Muslim 4345)
Mohammad aliamuru kuuliwa kwa mkongwe aitwaye Abu Afak. Hii ilitendeka miaka miwili baada ya Mohammad kuingia Medina. Abu Afak akikuwa na umri wa miaka 120. ‘kosa’ lake likiwa kuandika mashairi ya kukashifu vitendo vya mtume wa Uislamu-Mohammad vya kuchinja na kuteka wanawake vitani.
Mohammad akasema, “Ni nani ataniadhibia huyu mtwana?” Hivyo mfuasi wake Mohammad akainuka na kumuua Abu Afak. (Ibn Ishaq/Hisham 995).

Saturday, March 26, 2016

NZI, MIKOJO, NA MATE YA MUHAMMAD NI DAWA KATIKA UISLAM


UTATA WA KUJITIBU KATIKA UISLAM
1. Eti Nzi ni dawa?
2. Eti Mate ya Muhammad ni Dawa?
3. Eti Kunywa Mikoja ni dawa!!!!
Jamani hii sayansi ya Kiislam ilitokea wapi?
MUHAMMAD ASEMA NZI NI DAWA
"Kama nzi ataangukia kwenye kinywaji cha yoyote kati yenu, itafaa kumchovya (kwenye kinywaji), kwani moja ya mbawa zake ina ugonjwa na linguine lina tiba (kiuasumu cha ugonjwa) (1). Maelezo chini ya ukurasa (1) yanasema "Tazama Hadithi na.673 juzuu ya 7 (kwa maelezo)" Bukhari juzuu ya 4 kitabu cha 54 sura ya 15 na.531 kabla ya uk. 335.
"Abu Huraira alisimulia: Nabii alisema, ‘Kama nzi wa nyumbani ataangukia kwenye kinywaji cha mmoja wenu, na amchovye nzi huyo (kwenye kinywaji), kwani moja ya mbawa zake ina ugonjwa na nyingine ina tiba ya ugonjwa huo." Bukharijuzuu ya 4 kitabu cha 54 sura ya 16 na.537 uk.338.
Kwa taarifa, nzi aliyeshiba vizuri huenda haja kubwa kila baada ya dakika tano kwa mujibu wa
http://www.thebestcontrol.com/bugstop/control_flies.htm.
Abu Hureira ana kumbukumbu halisi: "Abu Huraira alisimulia: Nilimwambia Mtume wa Allah ‘Nimesikia simulizi (Hadithi) nyingi kutoka kwako lakini nimezisahau.’ Mtume wa Allah alisema, ‘Tandaza Rida (vazi) lako’ nilifanya kama alivyosema na kisha akaitembeza mikono yake kana kwamba anaijaza na kitu fulani (na kisha akaikunjua kwenye Rida langu) na kusema, ‘Chukua na jifunike shuka hili mwilini mwako.’ Nilifanya hivyo na baada ya hapo sijawahi kusahau kitu chochote." Bukhari juzuu ya 1 kitabu cha 3 sura ya 43 na.119 uk.89. Pia Bukhari juzuu ya 4 kitabu cha 56 sura ya 27 na.841 uk.538; Bukhari juzuu ya 9 sura ya 23 na.452 uk.332.
"Abu Huraira anasimulia: Mtume wa Allah alisema, ‘Ikiwa nzi ataangukia kwenye chombo cha yoyote kati yenu, mtu huyo na amchovye (kwenye hicho chombo) na kumtupa mbali, kwani kwenye bawa lake moja kuna ugonjwa na kwenye bawa linguine kuna uponyaji (1) (kiuasumu chake) yaani, tiba ya huo ugonjwa." Bukhari juzuu ya 7 kitabu cha 71 uk.58 na.673 uk.452-453.

Maelezo chini ya ukurasa (1) yanasema, "Kwa mujibu wa fani ya tiba sasa inafahamika sana kuwa nzi hubeba vijidudu vyenye kusababisha magonjwa (pathogens) kwenye baadhi ya sehemu zake kama ilivyosemwa na Nabii (karibu miaka 400 kabla wakati ambapo wanadamu walikuwa na ufahamu mdogo sana wa tiba ya kisasa). Kwa namna hiyo hiyo, Mungu aliumba viumbe na njia nyingine ambavyo vinaviua vijidudu hivi vinavyosababisha magonjwa k.m. kuvu la penisilini huua vijidudu kama Staphalococci na vinginevyo. Hivi karibuni majaribio yaliyofanywa chini ya usimamizi yameonyesha kuwa nzi hubeba vijidudu vyenye kusababisha magonjwa (pathogens) pamoja na viuasumu vya hivyo vijidudu. Kwa kawaida nzi anapogusa kimiminika kinachotumika kama chakula huathiri kimiminika kwa vijidudu vyake vinavyosababisha magonjwa, kwa hiyo ni lazima kumchovya ili kutoa pia kiuasumu cha vijidudu vyenye kusababisha magonjwa ili vipambane na vijidudu hivyo. Kuhusiana na somo hili, nilimwandikia pia rafiki yangu Dr. Muhammad M. El-SAMAHY mkuu wa Idara ya Hadithi ya Chuo Kikuu cha Al-Azhar Kairo (Misri) ambaye aliandika makala ya Hadithi hii na kuhusiana na fani ya tiba amesema kuwa wataalamu wa viumbe vidogo (mikrobiolojia) wamethibitisha kwamba kuna chembe chembe za chachu za longitudino zinazoishi kama vimelea ndani ya tumbo la nzi na chembe chembe hizi za chachu, ili kurudia mzunguko wao wa maisha huchomoza kupitia kwenye neli za kupumulia za nzi na endapo nzi atatumbukizwa tena kwenye kimiminika, chembe hizi hupasuka kwenye kimiminika na vitu vilivyomo ndani yake ni kiuasumu cha vijidudu vyenye kusababisha magonjwa ambavyo nzi huvibeba."

ALLAH KARUHUSU KULA NYAMA YA MIJUSI, FISI, NA NGAMIA


Ndugu msomaji,
Leo tutaandali nyama zinazo liwa na Waislam ambazo ni haram na Najisi kutokana na Biblia.
Mambo ya Walawi 7: 4 Pamoja na hayo, wanyama hawa hamtawala katika wale wenye kucheua, na katika wale walio na kwato; NGAMIA, kwa sababu yuacheua lakini hana kwato, yeye ni najisi kwenu. 6 Na SUNGURA, kwa sababu hucheua, lakini hana kwato, yeye ni najisi kwenu.
Lakini nilipo soma vitabu vya Kiislam, nikagundua kuwa, wao wana chuki kubwa na Nguruwe tu, huku wakila kwa furaha nyama ya Ngamia, mijusi, Sungura, Bata, nk.
Hebu tusome kidogo ushahid kutoka vitabu vyao:
Sayyidina Ibn Ammar (RA) alisema kuwa, siku moja alimuuliza Jabir Jbn Abdullah (RA) kuhusu uwindaji wa FISI. Alinijibu na kusema, inaruhusiwa kuwinda Fisi. Nilimuuliza, Je, tunaruhusiwa kula, na akanijibu kuwa Kula Fisi ni Halal (Inaruhusiwa kula Fisi).
Nikamuuliza tena, Je, Nabii wa Allah(SAW) aliruhusu kula Fisi? Jabir r alinijibu na kusema. NDIO, Nabii wa Allah aliruhusu kula Fisi. [Abu Dawud 3801, T 1798, Ibn e Majah 3085, Ahmedl4456]
9- Kitabu cha HAJJ
Kama tulivyo soma hapo juu, Waislam wameruhusiwa kula nyama ya Fisi. Zaidi ya hapo, Muhammad aliendelea na kuruhusu kula nyama za mijusi.
MTUME MUHAMMAD ASEMA KULA NYAMA YA MIJUSI NI HALAL
Sahih Muslim Kitabu 21, 4788 Idadi :
Ibn 'Umar taarifa kwamba kulikuwa na baadhi ya watu na Mtume wa Allah (amani iwe juu yake) miongoni mwa maswahaba wake alikuwepo Sad. Basi ililetwa nyama ya Mjusi na mwanamke miongoni mwa wake wa Mtume wa Mwenyezi Mungu (amani iwe juu yake) alisema: Ni nyama ya mjusi. Hapo Nabii Muhammad alisema: Kuleni hiyo nyama ya Mjusi kwa kuwa ni halali…
Eti kula Nguruwe ni haram lakini wanakula Fisi na Mijusi. Eti kula nguruwe ni haram lakini wanakula NGAMIA. Huu ni msiba.
Swali la kujiuliza, kama kweli Yehova Mungu wa Musa ndie huyo huyo Allah wa Waislam, kwanini WAISLAM wanapinga aya ya kula NGAMIA? Mambo ya Walawi 7: 4 Pamoja na hayo, wanyama hawa hamtawala katika wale wenye kucheua, na katika wale walio na kwato; NGAMIA, kwa sababu yuacheua lakini hana kwato, yeye ni najisi kwenu.
Zaidi ya hapo, Waislam wanakunywa Mikojo ya Punda na maziwa ya Punda. Je, huko si kuvynja amri ambayo ilisemwa katika Mambo ya Walawa 7 aya ya 4?
Abdallah Ibn Umar anasema kuwa kula Nyama ya Ngamia, na kunywa Maziwa yake ni HARAM. Lakini waislam wao wanaendelea kula Nyama ya Ngamia na kunywa Maziwa na Mikojo ya NGAMIA. (‘Abdallah Ibn ‘Umar al-Baydawi, Tafsir al-baydawi)
MUHAMAMD AWARUHUSU WAISLAM KUNYWA MIKOJO NA MAZIWA YA NGAMIA AMBAYE NI HARAMU KATIKA [WALAWI 7: 4]
Hata hivyo Muhammad aliwaamuru baadhi ya watu kumfuata mchungaji wake na kunywa maziwa na mikojo ya ngamia.

Friday, March 25, 2016

Prophet T.B. Joshua with Tanzanian President. Dr. John Magufuli


"A leader should rule in righteousness and in the fear of God so that he can be like a torch-light for everybody, a shining example." - T.B. Joshua
"When one rules over people in righteousness,
when he rules in the fear of God,
he is like the light of morning at sunrise
on a cloudless morning,
like the brightness after rain
that brings grass from the earth."
(2 Samuel 23:3-4)
Prophet T.B. Joshua with Tanzanian President. Dr. John Magufuli

BIBLIA INARUHUSU KULA NYAMA YA NGURUWE


JE, KULA NYAMA YA NGURUWE NI DHAMBI?
1. Je, kuna aya yeyote ile katika Agano Jipya inayo mkataza Mkristo kula nyama ya Nguruwe?
2. Je, kuna sheria yeyote ile kwenye Agano Jipya inayo kataza kula nyama ya Nguruwe?
3. Je, Yesu alisema au waamrisha Wafuasi wake wasile Nyama ya Nguruwe?
4. Je, Yesu alipo vitakasa vyakula vyote [Marko 7 :15-19] kunapingana na sheria ya hapo mwanzo kwenye Mambo ya Walawi?
Ndugu msomaji,
Katika hili somo, tutajifunza kuhusu ulaji wa Nyama ya Nguruwe na kwanini Wakristo wanakula Nyama ya Nguruwe.
Tuanze moja kwa moja kwa kusoma aya za Biblia:
"Bwana Mungu akambariki Nuhu na wanawe, akawambia Zaeni, mkaongezeke, mkaijaze nchi, kila mnyama wa katika nchi watawaogopa ninyi na kuwahofu, na kila ndege wa angani pamoja na viti vyote vilivyojaa katika ardhi,na samaki wote wa baharini vimetiwa mikononi mwenu, kila kiendacho kilicho hai kitakuwa chakula chenu, kama nilivyowapa mboga za majani ,kadhalika hivi vyote ,balo nyama pamoja na uhai ,yaani damu yake msile" {Mwanzo 9:1-4}
Ndugu msomaji wangu maandiko yamefunua wazi kwamba Mungu alitoa wanyama wote kuliwa baada ya mboga za majani walakini hatuoni Mungu akitoa sheria ama akiwabagulia wanyama wa kuliwa yaani walio safi na wasio safi, bali maandiko yametuonyesha kuwa Mungu alitoa wanyama wote kuwa chakula kwa wanadamu kama ilivyo shuhudiwa katika Mwanzo Mlango wa 9 aya ya 1-4.
Je sheria inayohusiana na wanyama safi na wasio safi ilitolewa wapi?
Ndugu msomaji kama ambavyo nilivyokwisha kutangulia kusema kuwa sheria hii inayohusiana na vyakula haikutolewa tangu mwanzo kwa ushaidi wa andiko ambalo nimekupa limeonyesha hivyo, swali la lini sheria hii ambayo ilihusiana na vyakula ilitolewa maandiko yapo wazi kabisa eneo ilo ni baada ya wana Israel kutolewa utumwani Misri ndipo tunaona katika biblia sheria inayohusiana na wanyama walio safi na wasio safi kwaiyo kabla ya hapo wanyama wote walikuwa chakula {Mambo ya Walawi 11 :1-7} kupitia fungu ili la biblia tunaona kuwa Mungu anatoa sheria inayohusiana na wanyama wanaopaswa kuliwa na wasiopaswa kuliwa?
Ni kweli kabisa Mungu alitoa hiyo kuwa ni sheria kwao wana wa Israel walakini tusiishie tu hapo katika kuangalia sheria kuwa ni sheria tusafiri pamoja kifikra,utakumbuka kuwa watu ambao kiasili sio wayahudi walikuwa hawana desturi za usomaji wa torati?
Je hii sheria iliyohusiana na wanyama safi na wasio safi ilifahamika kwao?
Bila shaka jibu ni hapana labda utajiuliza kwanini?
Napenda tujifunze ili jambo na kutokuacha historia ya vizazi pia na chanzo cha kusambaa kwa wanadamu duniani kote
Theolojia inatueleza kwamba vizazi vya ulimwengu huu vimetokana na wana watatu wa Nuhu ambao ni Shemu, Hamu, na Yafethi sasa katika historia ya chanzo cha mataifa mbalimbali kama inavyoelezwa kwamba wanadamu yaani mataifa yote yaliotokana na watoto wa Nuhu walikuwa wakiishi pamoja na walikuwa na lugha moja na usemi mmoja na waliishi pamoja, wanadamu hawa ikumbukwe kwamba hawakupewa sheria yoyote inayohusiana na wanyama wapasao kuliwa na wasiopaswa hawakupewa na hapa tunaelezwa ndio chanzo cha mataifa mbalimbali maana baada ya Mungu kuwachafulia lugha walisambaa kila mmoja mahali pake (Mwanzo 11:1-9}
Sasa swali la kujiuliza je wanadamu hawa waliondoka na ufahamu upi kuhusiana na vyakula, kwamba Nguruwe haramu ama?
Maana ifahamike kuwa kwao walipewa wanyama wote kuwa chakula kwa sababu hawakuwa na sheria inayohusiana na vyakula safi na visivyo safi kwao wanyama wote ni safi tu waliondoka na imani hiyo kama walivyopokea huu ndio ukawa mwanzo wa mpishano wa vyakula baina ya watu walioitwa wa mataifa na wayahudi baada ya wao kupewa sheria iliyohusiana na wanyama walio safi na waschakula.
Wayahudi walipata tabu sana kushiriki katika kalamu za watu ambao kiasili hawakuwa wasomaji wa torati na kuishi katika nchi zao, kwa sababu walipishana katika desturi za vyakula ,wayahudi hata wale ambao walikuja kuwa wafuasi wa Kristo walipata ugumu mno katika eneo ilo,sababu wao wayahudi walipewa sheria kuhusiana na wanyama safi na wasio safi ila mataifa kwao wanyama wote walikuwa safi sasa mtume Paulo hali akiwa na ufunuo wa Kimungu aliwaeleza wale wayahudi waliokuwa wakristo zama zile na walikuwa wakiambatana na mitume katika uinjilisti alisema maneno haya
" Kila kitu kiuzwacho sokoni kuleni, bila ya kuuliza uliza kwa ajiri ya dhamiri ,maana ,dunia ni mali ya Bwana na vyote viijazavyo, mtu asiyeamini akiwaalika ninyi mnataka kwenda ,kuleni kila kitu kiwekwacho mbele yenu bila ya kuuliza -uliza kwa ajili ya dhamiri" {1 Wakorintho 10:25-28}
Kwanini mtume Paulo awaagize wale kila kitu ikiwa wapo wanyama waliozuiliwa je alikuwa anapingana na Mungu? Lah hasha! hakuwa akipingana na Mungu, bali Mtume Paulo alifahamu kesi kuhusiana na vyakula, Yesu aliye kielelezo cha imani yetu aliitatua kupitia Marko 7 :15-19 pale alivyovitakasa vyakula vyote, akamaliza utata huo, hivyo baada ya hapo kila chakula kilikuwa halali kuliwa rejea tena kusoma Mwanzo 9:1-4
" Akawaambia hivi hata ninyi hamna akili ?
Hamfahamu ya kwamba kila kitu kilicho nje ya mtu, kikimwingia, hakiwezi kumtia mtu unajisi , kwa sababu hakimwingii moyoni, ila tumboni kisha chatoka kwenda chooni?
Kwa kusema hivi ali itakasa vyakula vyote ,akasema kimtokacho mtu ndicho kimtiacho mtu unajisi ,kwa maaana ndani ya mioyo watu hutoka mawazo mabaya ,uasherati,wivi uuaji,uzinzi, tamaa mbaya"
Kwa sababu Yesu alivitakasa vyakula vyote ndio maana tunaona agizo lake kwa Wayahudi aliokuwa akiambatana nao kwa ajili ya kueneza ujumbe wa Mungu kuwa wakialikwa katika majumba ya wasio amini na wakawapikia nyama ambazo mmezuiliwa msile na torati kuleni kwa sababu unajisi haupo ndani ya nguruwe wala ngamia ila unajisi upo mioyoni mwa watu
Ndugu pamekuwa na hoja juu ya nguruwe kuwa na madhara jamani kwani ni nguruwe tu ana madhara?
Je Ng'ombe hawa wa leo nyama zao hazina madhara?
Je Kuku wa kizungu na mayai yake hawa madhara kiafya?
Je chumvi za viwandani na mafuta pamoja na mavinywaji havina madhara?
Watu wa Mungu kimsingi kupitia Agano Jipya, Wakristo, hatuna sheria yoyote inayotuagiza kutokula Nguruwe hivyo basi sio dhambi kula Nguruwe ,dhambi katika tasfiri ya Biblia ya Union Version kupitia 1 Yohana 3:4 imetafsiriwa kuwa " dhambi ni uhasi wa sheria" kwaiyo ili dhambi iwepo lazima pawepo na uvunjifu wa sheria je katika agano jipya Wakristo tumepewa sheria inayotutaka kutokula Nguruwe ama ngamia kwa wanaokula?
Kama hakuna basi kula Nguruwe ama Ngamia sio dhambi?
Mungu tangia mwanzo alipotoa agizo la wanadamu kula nyama, alitoa wanyama wote kuwa chakula itakuwaje dhambi kwao?
Maana hakuwapa sheria iliyowabagulia wanyama wa kuliwa na wasio paswa kuliwa kwao wanyama wote walikuwa chakula sawa kama ambavyo Mungu ametoa wanyama wote kuwa chakula kwao, kama kweli alitaka wasiliwe nguruwe angewataza wasiliwe kabla hakuwapa wanadamu wanyama wote
Biblia inasema kila kiumbe cha Mungu ni kizuri, wala hakuna kiumbe cha kukataliwa ,kama kitapokelewa kwa shukrani ,kwa kuwa kimetakaswa kwa neno la Mungu na kwa kuomba {1Timotheo 4:4-5}
Kama hakuna kiumbe cha kukataliwa maana viumbe wote ni vizuri sasa ubaya wa Nguruwe ni nini?
Kama hacheuwi hii ndio sababu ndio Mungu ametaka awe hivyo!!!!!!! Ukianzia mistari ya juu utaona anaonya watu ambao wanawazuia wengine na baadhi ya vyakula kwa kisingizio cha wanyama wazuri na wabaya, sasa hawa leo ambao wanawataka watu kujitenga na baadhi ya vyakula tunawaweka kundi gani?
Biblia inasema viumbe vyote ni safi unganisha na Mwanzo 9:1-4 upate maana halisi, hivyo kula nguruwe sio dhambi ni halali kabisa
Sio vyakula ambavyo vinatuudhurisha mbele za Mungu tunakula kwa ajili ya miili yetu sio kwa ajili ya Mungu (Warumi 15:17 na Marko 7:15-19)
Hakuna kosa kula Nguruwe kwa mujibu wa Agano Jipya asanteni mbarikiwe nyote.
Mungu awabariki sana.
By permission: Pastor Samuel J. M, Christ Nations Org, Max Shimba Ministries Org, NKJV, Gideon Bible 1960, Green Island Tabernacle
Ni mimi Max Shimba, mtumwa wa Yesu Kristo,
For Max Shimba Ministries Org,
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2016. ALL RIGHTS RESERVED
Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.
March 25, 2016

Thursday, March 24, 2016

ALLAH KUPITIA MUHAMMAD AKIRI KUUMBA KWA SIKU SABA (7)

Ndugu msomaji,
Huu ni msiba mwingine kwa Waislam ambao kila kukicha Allah anawakoroga kwa kupitia Muhammad.
Bila ya kupotiza muda tuanze kwa kusoma sahihi hadith.
UTATA WA KWANZA:
ALLAH ALIUMBA DUNIA NA KILA KITU KWA SIKU SABA
Imetafsiriwa na Abu Hurairah; Nabii wa Allah alinishika Moono na akasema, Allah [Sifa zote na utukufu umwendee Allah] aliye umba dunia siku ya Jumamosi, na juu yake akaumba Milima siku ya Jumapili. Na akaumba Miti siku ya Jumatatu. Akaumba vitu mbalimbali siku ya Jumanne. Akumba Mwanga siku ya Jumatano. Akawajaza wanyama ndani yake siku ya Alhamisi na akamuumba ADAM, amani iwe juu yake baada ya alasir ya Ijumma, ikiwa ni uumbaji wake wa mwisho katika saa la mwisho la siku ya Injumaa, kati ya "Alasir na Usiku ulipoingia' (Muslim bin Hajjaj, as-Sahih, Hadith 7054 (27-2789)
Katika somo letu la leo, tutajifunza kuhusu uumbaji wa Dunia. Allah wa Uislam, anasema kuwa yeye ni Mungu na aliumba Dunia na vitu vyote vilivyo ndani yake. Hebu tuanze somo letu kwa kusoma aya za Quran.
UTATA WA PILI:
ALLAH ANAUMBA KWA SIKU SITA
Allah anasema katika Sura 7:54, 10:3, 11:7, na 25:59 kuwa, aliumba dunia kwa siku 6. Soma aya hizi hapa chini kwa ushaidi zaidi.
Quran 7:54. Hakika Mola Mlezi wenu ni Mwenyezi Mungu aliye ziumba mbingu na ardhi katika siku sita. Kisha akatawala juu ya Kiti cha Enzi. Huufunika usiku kwa mchana, ufuatao upesi upesi. Na jua, na mwezi, na nyota zinazo tumika kwa amri yake. Fahamuni! Kuumba na amri ni zake. Ametukuka kabisa Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wa viumbe vyote.
Surah 10: 3. Hakika Mola wenu Mlezi ni Mwenyezi Mungu, ambaye ameziumba mbingu na ardhi kwa siku sita, na ametawala kwenye ufalme wake, anaendesha mambo yote. Hapana mwombezi ila baada ya idhini yake. Huyo ndiye Mwenyezi Mungu, Mola wenu Mlezi. Basi muabuduni Yeye. Je! Hamkumbuki?
Lakini Ndugu zanguni, nilipo endelea kuchunguza Quran nikagundua kuwa, kumbe Allah alidanganya pale alipo sema kuwa aliumba Dunia kwa siku sita. Sasa ungana nami katika uchunguzi wa uumbaji wa dunia kama ulivyo wekwa kiuwazi zaidi kupitia Quran iliyo shushwa na Jibril.
Sasa tutasoma Surah ya 41: 9-12. Katika hizi aya tutakazo zisoma, utangudua kuwa Allah hakuumba Dunia kwa Siku 6 kama alivyo dai hapo mwanzoni.

UTATA WA TATU:
HII AYA INASEMA ALLAH KAUMBA KWA SIKU MBILI (2)
Quran 41:9. Sema: Hivyo nyinyi mnamkataa aliye umba ardhi katika siku mbili, na mnamfanyia washirika? Huyu ndiye Mola Mlezi wa walimwengu wote.
+ (Jumlisha)
HAPA ALLAH ANAUNGANISHA MAWINGU NA ARDHI KWA SIKU NNE(4)
Quran 41:10. Na akaweka humo milima juu yake, na akabarikia humo na akakadiria humo chakula chake katika siku nne. Haya ni sawa kabisa kwa wanao uliza 11. Kisha akazielekea mbingu, na zilikuwa moshi, akaziambia hizo na ardhi: Njooni, kwa khiari au kwa nguvu! Vyote viwili vikasema: Tumekuja nasi ni wat'iifu.
+ (Jumlisha)
HAPA ALLAH ANAZITENGENEZA MBINGU KWA SIKU MBILI (2)
Quran 41:12. Basi akazifanya mbingu saba kwa siku mbili, na akazipangia kila mbingu mambo yake. Na tukaipamba mbingu ya chini kwa mataa na kwa ulinzi. Hichi ndicho kipimo cha Mwenyezi Mungu Mwenye Kujua.
HIZI ZOTE KWA PAMOJA NI SIKU NANE (8)
Siku mbili kwa ajili ya viumbe wa dunia, basi siku nne kujaza ardhi na milima baraka, na chakula kwa ajili ya wakazi wake wote, na mwisho kwa siku mbili zaidi ili kujenga mbingu saba na kujenga nyota yao. Hii inaongeza hadi 2 + 4 + 2 = siku 8 kinyume na siku 6 zilizotajwa katika aya nyingine.
NGOJA NIWEKE KWA UFUPI
Muundo ni wazi sana: Haya ni Matabaka Matatu ambayo ni umbaji chini hadi juu:

A = SIKU MBILI:
Quran 41:9*** Mbingu [angani, "dari" juu ya dunia] katika siku 2
----------

B = SIKU NNE:
Quran 41:10*** BARAKA [kujaza dunia na kila kitu zinahitajika kwa ajili ya maisha] katika siku 4
---------

C = SIKU MBILI:
Quran 41:12***EARTH [msingi] kukamilika katika siku 2
SASA JUMLISHA HIZO SIKU:
A + B + C = 2 + 4 + 2 = 8
Ndugu zanguni, hivi Allah alishindwa mahesabu au ndio kutuhakikishia kuwa yeye hakuwa Muumbaji? Kwanini Allah afanye makosa makumbwa namna hii? Leo Allah kwa mara nyingine tena ametuhakikishia kuwa yeye si Muumbaji. Uchaguzi ni wako, kufuata Allah asiye fahamu aliumba Dunia kwa Siku Ngapi au Jehova ambaye alisema aliumba Dunia kwa siku 6.
Zaidi ya hapo, Allah anasema kupitia Muhammad (Muslim bin Hajjaj, as-Sahih, Hadith 7054 (27-2789) kuwa, aliumba kila kitu kwa siku SABA. Hapo sasa mimi sina la ziada, nawaachia wenyewe mjadili, JE ALLAH ALIUMBA AU NI LONGA LONGA TU?
Mungu awabariki sana.
Ni mimi Max Shimba, mtumwa wa Yesu Kristo,
For Max Shimba Ministries Org,
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2016. ALL RIGHTS RESERVED
Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.
March 24, 2016

Tuesday, March 22, 2016

MTUME MUHAMMAD ALIKUWA ANADAI SADAKA - FEDHA KABLA YA KUONGEA NAE

Ndugu msomaji,
Leo nitajibu hoja ambayo Waislam wamekuwa wakiitumia kwa muda mrefu kuwashutumu Wakristo kuwa tunadai Sadaka kutoka waumini, huku wakificha aya kutoka Quran zinazo onyesha kuwa Muhammad alikuwa anapokea Sadaka.
Watu waliokuwa wakiishi katika zama za Mtume walikuwa wanaenda kwa Mtume katika nyakati tofauti, na walikuwa wanamuuliza masuala tofauti yenye faida na yasiyo na faida, na suala hili lilisababisha kumkosesha Mtume wakati wa mapumziko, ndipo ilipokuja Qur-ani na kuwaamrisha watu kuwa kila anayetaka kuuuliza suala basi kwanza anatakiwa kutoa sadaqa, kabla ya kuuliza suala lake. Na Aya hiyo iko katika (Surat Mujadila aya ya 12) inasema hivi:-
يَا اَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِذَا نَاجَيْتُمُ الرَّسُولَ فَقَدِّمُوا بَيْنَ يَدَيْ نَجْوَاكُمْ صَدَقَةً ذٰلِكَ خَيْرٌ لَّكُمْ وَاَطْهَرُ فَإِن لَّمْ تَجِدُوا فَإِنَّ اللهَ غَفُورٌ رَّحِيمٌ[1]
Maana ya Aya hiyo ni kama hivi ifuatavyo:-
“Enyi mlioamini! Mnapomsemesha Mtume Muhammad toeni Sadaqa kabla ya kumsemeza; hayo ni bora kwenu na ni ya kukusafisheni sana. Ikiwa hamkupata (cha kutoa), basi Mwenyeezi Mungu ni Mwingi wa kusamehe (na) Mwingi wa kurehemu”.
Kwa amri hiyo basi, wao wenyewe wakawa ni wenye kurudi nyuma, na ni mtu mmoja tu ndiye aliyekwenda kwa Mtume (s.a.w.w), na kumuuliza masuala baada ya kushuka Aya hii, naye alitoa dirham kumi, kisha akauliza masuala muhimu ya kidini mbele ya Mtume (s.a.w.w). Naye alikuwa ni Dinar ambaye ni Mtumishi wa Imam Ali bin Abi Talib (a.s).
Lakini watu walipo gundua kuwa Muhammad alikuwa mtume bandia na anatumia sadaka kulisha famila yake kubwa, Allah akashusha aya kama ifuatavyo, nayo ni (Aya ya 13 ya Surat Mujadilah) isemayo:-
اَاَشْفَقْتُمْ اَن تُقَدِّمُوا بَيْنَ يَدَيْ نَجْوَاكُمْ صَدَقَاتٍ فَإِذْ لَمْ تَفْعَلُوا وَتَابَ اللهُ عَلَيْكُمْ فَاَقِيمُوا الصَّلاَةَ وَآتُوا الزَّكَاةَ وَاَطِيعُوا اللهَ وَرَسُولَهُ وَاللهُ خَبِيرٌ بِمَا تَعْمَلُونَ[2]
Maana ya Aya hiyo ni kama hivi ifuatavyo:-
“ Oh! Mnaona tabu kutanguliza hiyo Sadaqa kabla ya kumsemeza kwenu? Ikiwa hamjafanya haya basi. (Yamekwisha hayo). Na Mwenyeezi Mungu amekusameheni. Basi simamisheni sala na toeni Zaka na Mtiini Mwenyeezi Mungu na Mtume wake. Na Mwenyeezi Mungu anayo habari ya mnayoyatenda yote”.
Kama tulivyo soma hapo kwenye Surat Mujadilah aya ya 13, Muhammad kagonga mwamba, baada ya Waarabu kumshtukia kuwa Muhammad alikuwa anakula fedha zao kwa kuwapa unabii wa uongo.
Hebu soma kwanza:
17. SURA AL ISRAAI (BANI ISRAIL)
90. Na walisema: Hatutakuamini mpaka ututimbulie chemchem katika ardhi hii.
91. Au uwe na kitalu cha mitende na mizabibu, na utupitishie mito kati yake ikimiminika.
92. Au utuangushie mbingu vipande vipande kama ulivyo dai; au utuletee Mwenyezi Mungu na Malaika uso kwa uso.
93. Au uwe na nyumba ya dhahabu, au upae mbinguni. Wala hatutaamini kupaa kwako mpaka ututeremshie kitabu tukisome. Sema: Subhana Rabbi, Ametakasika Mola wangu Mlezi! Kwani mimi ni nani isipo kuwa ni mwanaadamu na Mtume?
(Qur-Sura 17:90-93)
Baada ya kuombwa afanye angalau muujiza mmoja tu, Muhammad alishindwa vibaya sana na kuto fanya hata muujiza mmoja.
Swali:
1. Kwanini Muhammad alishindwa kufanya miujiza kama alivyo ombwa afanye?
2. Muhammad ni Nabii peke yake alieshindwa kufanya Miujiza tokea dunia iumbwe, Je, anaa kufuatwa na kuaminiwa?
3. Kwanini Allah nay eye hakumsaidia Nabii wake kufanya muujiza?
HAKIKA MUHAMMAD ALIKUWA NABII WA UONGO
Mungu awabariki sana.
Ni mimi Max Shimba, mtumwa wa Yesu Kristo,
For Max Shimba Ministries Org,
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2016. ALL RIGHTS RESERVED
Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.
March 22, 2016

JINSI YA KUTOA PEPO WABAYA/CHAFU

Ndugu msomaji,
Maana ya neno pepo linamaanisha, pepo mbaya, shetani, mwovu, mharibifu na mwangamizi. Hao ni malaika waliomuasi Mungu wakatupwa duniani. “Kulikuwa na vita mbinguni; Mikaeli na malaika zake wakapigana na Yule joka (Shetani), Yule joka naye akapigana nao pamoja na malaika zake; Nao hawakushinda, wala mahali pao hapakuonekana tena mbinguni. Yule joka akatupwa, Yule mkubwa, Yule wa zamani, aitwaye Ibilisi na Shetani, audanganyaye ulimwengu wote; akatupwa hata nchi, na malaika zake wakatupwa pamoja naye.” Ufunuo 12:7-9.
1. Ili kutoa pepo, kuna mambo ambayo yanapaswa kuzingatiwa:
Ni lazima uwe na nguvu za Roho Mtakatifu.Tunaweza kujifunza kwa Yesu alivyoweza kutoa pepo kwa uwezo na nguvu za Roho. Imeandikwa, “…..awaaamuru pepo wachafu kwa uwezo na nguvu, nao hutoka.” Luka 4:36.
2. Kutoa pepo kwa jina la Yesu. Aliye na amri na mamlaka ya kutoa pepo ni mkristo ambaye amemwamini Yesu Kristo kuwa Bwana na mwokozi wa maisha yake. “Na ishara hizi zitafuatana na hao waaminio; kwa jina langu watatoa pepo……” Mathayo 16:17. Wale ambao bado hawajamwamini Yesu na kuokoka, Si vyema kujaribu kutoa Pepo kwa sababu hatatoka, vile vile wanaweza kushambuliwa na hao walio na Pepo, kama wale wana wa Skewa, Kuhani Mkuu.
“.....wakajaribu kutaja jina la Bwana Yesu juu yao waliopagawa na pepo wachafu, wakisema, Nakuapisha kwa Yesu, Yule anayehubiriwa na Paulo. Walikuwako wana saba wa mtu mmoja Skewa, Myahudi, Kuhani Mkuu, walifanya hivyo..... na yule mtu aliye pagawa na pepo wachafu akawarukia wawili, akawaweza, akawashinda, hata wakatoka mbio katika nyumba ile hali wa uchi na kujeruhiwa.” Matendo 19:13-16.
3. Kufanya maombi kila siku na wakati mwingine kufunga. Bila kufanya hivyo haiwezekani kwa neno lolote, ndio maana Yesu alisema “Lakini kwa namna hii haitoki ila kwa kusali na kufunga.” Mathayo 17:21.
4. Kutoa pepo kwa imani. Unaweza kujifunza kwa wale wanafunzi wa Yesu waliposhindwa kumtoa pepo Yule kijana. Walishindwa kwa sababu ya upungufu wa imani. Wangekuwa na imani wangeweza kumtoa Yule pepo. “Kisha wale wanafunzi wakamwendea Yesu kwa faragha wakisema, mbona sisi hatukuweza kumtoa? Yesu akawaambia kwa sababu ya upungufu wa imani yenu…..” Mathayo 17:19-20.
5. Kutoa pepo kwa amri na mamlaka. Unaamuru kwa jina la Yesu atoke naye hutoka. Tunaweza kujifunza kwa Mtume Paulo alivyomtoa pepo Yule kijakazi, akaamuru kwa kumwambia Yule pepo, “..…nakuamuru kwa jina la Yesu Kristo mtoke huyu, Akamtoka saa ile ile.” Matendo 16:18.
6. Makosa yanayofanyika kwa wale ambao wanakemea pepo, kwa kuwaambia ninakuangamiza kwa damu ya Yesu, ninakuteketeza kwa moto, au ninakufunga. Kufanya hivyo ni kinyume na mamlaka ya Mungu aliyowapa watoto wake. Kwa sababu hiyo, Mungu hajatupa mamlaka ya kuwaangamiza, Kuwateketeza, wala kuwafunga. Bado pepo watakuwepo katika dunia hii kwa sababu wakati wao wakuhukumiwa na kuteswa haujafika. Ndio maana pepo walipomuona Yesu, “…..wakasema,Tuna nini nawe, Mwana wa Mungu? Je! Umekuja kututesa kabla ya muhula wetu?” Mathayo 8:23.
7. Wakati wa kumhudumia mwenye pepo si sahihi au lazima kuongea na mapepo na kuwaliza maswali wametoka wapi, nani akawatuma, ni kwa nini wanamtesa huyo mtu, ingawa kuwauliza maswali kunaweza kukupa ufunuo fulani. [Yesu Akamkemea, Akisema, fumba kinywa, umtoke. Yule pepo mchafu akamtia kifafa, akalia kwa sauti kuu, akamtoka( Marko 1:25-26).] Hatupaswi kumsikiliza shetani na mapepo yake kwa sababu wao ni waovu na waongo siku zote. “....Asemapo uongo husema yaliyo yake mwenyewwe; kwa sababu yeye ni mwongo, na baba wa huo” Yohana 8:44. Yesu Kristo hakufanya hivyo ambaye ndiye kielelezo chetu katika utumishi, ijapokuwa alimwona yule mtu aliyekuwa amepagawa na kuteseka siku nyingi alimuuliza swali akitaka kujua jina lake, si jina la pepo.Badala yake pepo waliokuwa wamemtawala yule mtu walijibu wao ni jeshi. “Yesu akamwuliza jina lako nani? Akasema jina langu ni jeshi; kwa sababu pepo wengi wamemwingia”. Luka 8:30.
Pepo atolewapo hutaka kurudi.
Pepo anapotolewa ndani ya mtu aliyempagawa huondoka na baadae hurudi na kuangalia kama anaweza kuingia tena.Ikiwa mtu huyo anaishi maisha ya dhambi huona nyumba ni chafu na kuingia."Pepo mchafu amtokapo mtu, hupitia mahali pasipo maji, akitafuta mahali pa kupumzika, aspate. Halafu husema, nitarudi nyumbani kwangu nilikotoka; hata akija aiona tupu, imefagiwa, na kupambwa. Mara huenda akachukua pepo wengine saba walio waovu kuliko yeye mwenyewe, nao huingia na kukaa humo; na mtu yule hali yake ya mwisho huwa mbaya kuliko ya kwanza. Ndivyo itakavyokuwa kwa kizazi hiki kilicho kibaya". Mathayo 12:43-45.
MAMLAKA YA KUTOA PEPO UMEPEWA NA YESU
Marko 16:17-18 inasema, "ishara hizi zitafuatana na hao waaminio; kwa jina Langu watatoa pepo...." Kila Mkristo anao uwezo wa kuwatoa pepo! Sio swala la kwamba "una nguvu" kiasi gani au jinsi gani upo "kiroho" ; cha muhimu ni kuwa Yesu Amekupa mamlaka Yake; unatembea katika jina Lake.
Shetani hana haki ya kuendesha mambo katika maisha yako, au nyumbani mwako au katika maisha ya wale uwapendao. Tumia mamlaka yako katika Kristo dhidi yake.
JE, NI WAKATI GANI UNAWEZA TOA PEPO
Unaweza kuwatoa pepo siku yoyote, muda wowote na mahala popote, kwa kutumia jina la Yesu tu. Usijadiliane naye; mtoe!
Unaweza ukajiuliza. "Nitajuaje kuwa pepo ametoka ninapomkemea?" Hilo ni rahisi. Yesu Alisema, unapowaambia pepo watoke, hutoka. Neno Lake Linakamilisha hilo. Kazi yako ni kumkemea pepo atoke, na jukumu lake pepo ni kutii.
Ingawa, wakati mwingine pepo hujionesha na kulia kwa sauti pindi wanapomtoka yule mtu unayewatoa kwake. Mfano ni kama tulivyosoma katika mstari wetu wa ufunguzi. Pia tunaona tukio kama hilo katika matendo 8:6-8 pale Filipo alipomuhubiri Kristo kwa watu: "...pepo wachafu wakawatoka wengi waliopagawa nao, wakilia kwa sauti kuu..."
NINI KINAWEZA TOKEA WAKATI WA KUTO PEPO
Hivyo, katika kutoa pepo, roho waovu huweza kupiga yowe na kelele kwa kuteseka pindi wanapotoka; na kisha badiliko la wazi kwa wale ambao pepo wamewatoka hujionesha kuwa kuna tofauti.
Hata hivyo, haijalishi pepo wamepiga yowe au kelele wakati ulipowakemea; cha muhimu ni kile Yesu Alichokisema,"...kwa jina Langu mtatoa pepo..."( Marko 16:17). Huo ndiyo uhalisia, na unapaswa kuwa ndiyo msingi wa imani yako. Hivyo, unapowakemea pepo, wanakuwa hawana chaguo lolote- zaidi ya kukimbia.
Somo Zaidi:
Luka 10:18-19 Akawaambia, Nilimwona shetani, akianguka kutoka mbinguni kama umeme. Tazama, Nimewapa amri ya kukanyaga nyoka na ng'e, na nguvu zote za yule adui, wala hakuna kitu kitakachowadhuru.
Matendo 16:16-18 Ikawa tulipo kuwa tukienda mahali pale pa kusali, kijakazi mmoja aliyekuwa na pepo wa uaguzi akatukuta, aliyewapatia bwana zake faida nyingi kwa kuagua. Akamfuata Paulo na sisi akipiga kelele, akisema watu hawa ni watumishi wa Mungu Aliye juu, wenye kuwahubiria Njia ya wokovu. Akafanya hayo siku nyingi. Lakini Paulo Akakasirika, akageuka akamwambia yule pepo, nakuamuru kwa jina la Yesu Kristo, mtoke huyu. Akamtoka saa ile ile.
Ndugu msomaji,
Nategemea umesha elewa kuwa, umepewa haki ya kuyatoa MaPepo, na anza kulitoa pepo ambalo linakusumbua, Ndio, unaweza kutoa pepo yako chafu. Biblia inasema kuwa (Marko 16:17-18) = [Ishara hizi zitawafuata Waaminio, watatoa pepo"], umepewa Mamlaka ya kutoa pepo, sio pepo wa mwenzako tu, la hasha, hata pepo ambayo imo ndani yako.
Mamlaka unayo na anza kufanya kazi ya Bwana.
Mungu akubariki sana,
Ni mimi Max Shimba, mtumwa wa Yesu Kristo,
For Max Shimba Ministries Org,
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2016. ALL RIGHTS RESERVED
Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.
March 22, 2016

ALLAH AFANYA KOSA KUBWA LA KISAYANSI NA JIOGRAFIA KUHUSU KUTUA/ZAMA KWA JUA



Ndugu msomaji,
Zul-Qarnain na Kutua kwa Jua katika Sura 18:85-86
Je, ni kweli kuwa jua linazama katika chemichemi za maji zenye tope au giza, au Koran ina makosa, au kuna maelezo mengine? Kwanza tutaangalia maana ya wazi Sura ya 18:85-86, na kisha tutaangalia maelezo na majibu ya baadhi ya Waislam kuhusu jambo hili.
Unajimu Kidogo
Inawezekana kuwa haijulikani kwa mapana kwamba watawala wa kislam wa Abbasid, Waarabu na Waajemi waliendelea sana katika unajimu, wakizipa majina nyota nyingi, hata walinukuru na kusahihisha baadhi ya orodha za hesabu za watawala wa Misri (Ptolemy’s tables). Hata hivyo jua ni kubwa mara nyingi zaidi ya dunia nzima, na dunia husafiri ikilizunguka jua. Jua halizami katika chemichemi za maji zenye tope.
Zul-Qarnain ni Nani?
Hatuna ushahidi kama Muhammad alimwambia mtu yeyote kuwa Zul-Qarnain alikuwa nani hasa. Waislam wana mitazamo minne tofauti.
Alexander Mkuu (wa Makedoni) ni mtazamo wa Waislam wengi zaidi. Zul-Qarnain humaanisha kuwa ni "mtu mwenye pembe mbili." Kuna hadithi ya kubuniwa isemayo kuwa Alexander Mkuu alikuwa mungu na alikuwa na pembe mbili za kondoo dume zilizokuwa zinakua pembeni mwa kichwa chake. Licha ya ukweli kwamba hii haikuwa kweli (na ni tatizo kupata kofia ya vita—helimeti inayoweza kutosha), hadithi hii ilijulikana, na waislam wengi hudhani kuwa Allah katika sura ya 18 Alexander alitajwa kwa jina hili, mungu.
Koreshi I Muajemi ni mtizamo mwingine. Ufalme wake hasa ulikuwa ufalme uliohusisha makundi mawili: Wamedi na Waajemi, lakini zaidi ya hayo hakuna uthibitisho kuwa pembe mbili zinamhusu yeye.
Mfalme wa Yemeni ambaye alivaa kofia ya vita yenye pembe mbili za kondoo dume, ni mtazamo walionao baadhi ya Waislam.
Mtu asiyejulikana ni mtizamo wa nne. Hata hivyo inaonekana si vema sana kutoa maelezo juu ya watu ambao msemaji hajawahi kuyasikia.
Hitimisho: Haijalishi kuwa Zul-Qarnain alikuwa nani hasa. Kama aligundua kuwa jua hutua kwenye chemichemi za maji zenye tope, na huwa halizami kwenye chemichemi za maji zenye tope, kwa hiyo huu ni ubatili, bila kujali mtu ambaye Muhammad alimzungumzia.
Sura 18 Mawazo na Majibu

Wazo la I: Jua huzama kwenye chemichemi za maji zenye tope!
Kwa Waislam wa awali, Koran iliwafundisha kuwa jambo hili linatokea hasa. Mwanahistoria wa kiislamu wa awali al-Tabari juzuu ya 1 uk.234 anaonesha hili. Kama mfano wa pili, "[Dhu al-Qarnaiyn] alishuhudia kuzama kwa jua katika sehemu yake ya kupumzika ndani ya bwawa jeusi na tope la kunuka." Kwa mujibu wa al-Tabari juzuu ya 5 uk.173-174. Dul Qarnain [Zul Qarnain] anapatikana pia kwenye al-Tabari juzuu ya 1 uk.371.
Jambo jingine linaloingiliana na hili, dunia hukaa juu ya samaki mkubwa kwa mujibu wa al-Tabari juzuu ya 1 uk.220 (839-923 K.K.).
Wazo la 2: Jua lilionekana kwa Alexander likitua katika ziwa la Ithaca Makedonia
Wazo hili hubashiri kuwa Zul-Qarnain alikuwa Alexander, na kwamba Alexander alikuwa Muislam mzuri. Wazo hili haliendani na ukweli kwamba Alexander alikuwa na hekalu lililotengenezwa kwa ajili yake. Pia Alexander alikwenda kuteka kaskazini na magharibi mwa Ithaca ambayo ni Albania ya sasa.
Kibaya zaidi katika wazo hili, Wayunani walifanya makazi mamia ya maili magharibi mwa Ithaca ambayo ni Hispania, Sicily, n.k. za asa, miaka mia tano kabla ya Alexander. Kitu gani kingemfanya Myunani mwenye akili sana afikiri kuwa jua lilizama katika ziwa la Makedonia wakati meli za kiyunani zilikuwa zinaenda mbali zaidi magharibi mwa nchi ya Alexander? Kwa nyongeza, Tertullian katika Hoja Juu ya Nafsi [A Treatise on the Soul] sura 49 uk.227 anasema kwamba Aristotle, aliyeishi wakati ule ule, anataja shujaa kutoka kisiwa cha Sardinia mbali magharibi mwa Makedoni lakini ni kama kwenye latitudi ile ile.
Wazo la 3: "Chemichemi ya maji yenye tope" ni Bahari ya Atlantic
Bahari ya Atlantic haina tope na si nyeusi, bali ni bluu-kijani. Pia si chemichemi bali ni bahari. Jua huwa halizami katika bahari. Cha muhimu zaidi, Alexander, Koreshi I wa Uajemi na wafalme wa Yemeni hawakuwahi kwenda kwenye Bahari ya Atlantic na Sura ya 18:85-86 inasema kuwa Zul Qarnain aliona au alishuhudia hili.
Sababu yoyote kati ya hizi nne inatosha kulindoa wazo hili, hivyo basi kwa Waislam wanapendekeze hili? Hiki ndicho kiwango ambacho wanajaribu kwenda ili kuonyesha kuwa Sura ya 18:1-2 sio potofu. Ikiwa Allah [Mungu] wa uislam alikuwa na wazo hili katika Koran, na Allah alijua kuwa hili ni wazo potofu, hivyo jambo hili litakuwa uongo. Kama Allah wa uislam hakujua ukweli huu, wasingelikuwa na ufahamu na hakika wasingekuwa na uwezo wa kujua kila kitu. Kama mistari hii isingetoka kwa Allah [Mungu] wa uislam, basi Koran ingekuwa na makosa dhahiri, kwa sababu inathibitisha upotofu huu kutoka kwa Allah wakati sivyo hivyo. Bila shaka, ikiwa kweli si Allah wa uislam, na Mungu wa kweli si mwandikishi wa Koran, basi Allah wa uislamu hakusema uongo kwa sababu hayupo.
Wazo la 4: "Chemichemi ya maji yenye tope" ni Koreshi I alikoangalia Bahari Nyeusi (Black Sea)
Hata kama Koreshi I alikwenda magharibi mwa ufuko wa mashariki mwa Bahari Nyeusi (Black Sea), na jua lingeonekana vipi likitua katika Bahari Nyeusi, ikiwa alikuwa ameshaupita ufuko wa mashariki kuelekea kusini na mashariki? Hatuna ushahidi kuwa Koreshi aliwahi kusafiri kwenda ukanda unaojumuisha Georgia, Amernia, Azerbaijan, n.k. za sasa, zilizo mashariki mwa Bahari Nyeusi. Muislam angekuwa na hoja yenye udhaifu kidogo kama angesema kuwa Koreshi aliliona jua likichomoza kutoka kwenye Bahari Nyeusi, kwa sababu alivuka hadi Uyunani, lakini Koran inaongelea kuzama kwa jua. Hata hivyo Bahari Nyeusi sio chemichemi, kila mtu kuanzia wamisri na wengineo kaskazini ya mbali, walijua kuwa jua halikuzama kwenye Bahari Nyeusi.
Wazo la 5: "Chemichemi ya maji yenye tope" ni Koreshi I alikoangalia Bahari ya Aegean
Lakini Waajemi walikuwa wakiwafahamu vema Waatene, Waspartani, (asili ya Wayunani), na Wayunani wengine. Waajemi wangelijua kuwa Wayunani hawakuwa upande mwingine wa jua.
Wazo la 6: Hakika "Chemichemi ya maji yenye tope" ni mfalme wa alikoangalia Bahari Nyekundu
Wayemeni (Wasaba/Waseba) wakati wote waliwafahamu Waabisinia (Waethiopia) ng’ambo ya mto. Ikiwa walifikiri kuwa jua lilizama katika Bahari Nyekundu (Red Sea) basi Waabisinia wangelikuwa watu waliokuwa upande mwingine jua lilikokuwa.
Wazo la 7: "Chemichemi ya maji yenye tope" ni usemi wa kufananisha na kitu kingine
Ikiwa kitu hiki hakikuwa halisi, bali ni kifananishi cha kitu au vitu vingine, basi Koran imeshindwa kuelezea kuwa hakikuwa kweli, na wazo hili lilikuwa la kupotosha. Zaidi ya yote, hakuna mtu anayeweza kusema kwa hakika kuwa kitu hiki kilifananishwa ni nini hasa.
Hakuna kitu chochote kwenye Koran kinachoonyesha kuwa kitu hiki si halisi, na Waislam wengi wa awali walikichukulia kuwa kitu halisi, yaani ukweli halisi. Kwa kuzingatia kuwa walijua maana hasa ya jambo hili kutoka kwa wafuasi wa Muhammad, kwa hiyo walipotoshwa na Sura ya 18.
Wazo la 8: Muhammad alikuwa akisimulia juu ya ndoto yake
Wazo hili halimfahamu Zul-Qarnain kuwa ni nani hasa. Ikiwa Muhammad alikuwa anasimulia juu ya ndoto yake, jua lingeweza kutua popote alipotaka litue. Hata kama haifahamiki ni muhusika gani dhahania aonaye kitu kilicho potofu kabisa, na watu wanaoamini kuwa ni kitu cha kweli, atatufundishaje sisi juu ya kuiamini kweli.
Hata hivyo, ikiwa mtu atasema kuwa walimwona mtu fulani aitwaye ‘Ali akifanya kitu cha ajabu ajabu, na mamilioni ya watu wakamwamini kwa karne nyingi. Je, mtu huyo ataweza kuwa mwongo ikiwa alisahau kuwaambia watu kwamba, "ilikuwa ndoto yangu tu na sikumwona Ali akifanya hivyo kwa macho yangu."?
Hitimisho
Bila kujali kama Zul-Qarnain alikuwa Alexander Mkuu au mtu mwingine, Korani yaeleza jambo hili kama ukweli kuwa jua huzama katika chemichemi za maji yenye tope. Hata watu wa zamani miaka 1,000 kabla ya Muhammad walijua kuwa jua halikuzama upande huu wa Hispania. Wazo hili halikuwa kifananishi cha kitu kingine kwa sababu hakuna Muislam wa zamani aliyepatikana kuwa hakulichukua jambo hili kuwa halisi au kutoa maana yake kama usemi wa kufananisha na kitu kingine, na Waislam wote wa zamani waliamini kuwa Koran haikutolewa kwa ajili ya kudanganya.
Orodha ya Vitabu vya Tafsiri ya Korani
1. Arberry, Arthur J. The Koran Interpreted. Macmillian Publishing Co., Inc. 1955.
2. Dawood, N.J. The Koran. Penguin Books. 1956-1999.
3. Malik, Farooq-i-Azam. English Translation of the Meaning of AL-QUR’AN : The
Guidance for Mankind. The Institute of Islamic Knowledge. 1997
4. Pickthall, Mohammed Marmaduke. The Meaning of the Glorious Koran. Dar al-
Islamiyya (Kuwait) (no date given)
5. Rodwell, J.M. The Koran. First Edition. Ivy Books, Published by Ballantine
Books. 1993.
6. Shakir, M.H. The Qur’an. Tahrike Tarsile Qur’an, Inc. 12th U.S. Edition 2001.
7. Sher Ali, Maulawi. The Holy Qur’an. Islam International Publications Limited
(Ahmadiyya) 1997
8. Yusuf ‘Ali, Abdullah. The Holy Qur-an : English translation of the meanings
and Commentary. King Fahd Holy Qur-an Printing Complex. (Al Madina
Saudi Arabia) 1410 A.D.
Vitabu Vingine vya Rejea
Encyclopaedia Britannica. Encyclopaedia Britannica, Inc. 1958.
The History of al-Tabari : An Annotated Translation. Ehsan Yar-Shater, General Editor. State University of New York Press 1989-
Mungu awabariki sana.
Ni mimi Max Shimba, mtumwa wa Yesu Kristo,
For Max Shimba Ministries Org,
MAX SHIMBA MINISTRIES ORG ©2016. ALL RIGHTS RESERVED
Everyone is permitted to copy and distribute verbatim copies of this license document, but changing it is not allowed.
March 22, 2016

FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE

  **URGENT UPDATE**   **FORMER MUSLIM EVANGELIST MUSA BELLO ARRESTED BY NIGERIAN POLICE** Shimba TV, New York has received distressing news ...

TRENDING NOW